QUR-ANI KATIKA MAISHANI MWETUDeprecated: Function eregi_replace() is deprecated in /home/swaalshia/public_html/page.php on line 99 Deprecated: Function split() is deprecated in /home/swaalshia/public_html/page.php on line 103 BISMILAHI RAHMANI RAHIYMI KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU QUR_ANI NDANI YA MAISHA YA MWANAADAMU Qur’ani tukufu na Hadith, ndivyo vitu viwili vya kimsingi ambavyo vinaunda Sheria za Kiislamu na kuzihakikisha, na ni kutokana na vitu viwili hivyo ndipo misingi yote ya dini inaporejea. Hata hivyo, ni Qur’ani tukufu tu ndiyo marejeo makubwa ambayo Hadith zinategemea. Kwa ajili hiyo, Hadith hazitofautiani au kupingana na Qur’ani ambayo inaaminiwa kuwa ndiyo asili ya ukweli wote. Miongoni mwa maudhui yenye maana Kwa maana hiyo Qur’ani imehifadhi haki za kila mmoja, na za jamii, imefanya kuenea kwa uadilifu, imewapa watu moyo wa kuishi pamoja kwa ushirikiano na ihsani, na imeweka kipimo cha kumcha Mwenyezi Mungu kuwa ndiyo tofauti pekee baina ya watu. Hadith ni chochote kile ambacho Mtume (s.a.w.w.) amekitenda na ambacho si Qur’ani; au mambo ambayo yamemfikia kupitia kwa ufahamu wake au maono, na kuthibitishwa na Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo (Sunnah) inakusanya vitendo na maneno yanayohusika na ufafanuzi wa itikadi, Swala au ibada nyinginezo, pia kulingana na uhusiano mwema baina ya ndugu, kumfundisha mwenendo mzuri, na kuamrisha mambo mema na kukataza maovu. Kwa hivyo chochote kilichotendwa na Mtume (s.a.w.w) katika hali kama hiyo, huchukuliwa Malezi ya Watoto katika Uislamu Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Hakika mimi ni mwanaadamu, pindi nitakapowaamrisha jambo linalohusiana na dini yenu, lifuateni, na nitakapowaamrisha jambo kutokana na maoni yangu, basi kumbukeni kuwa mimi ni mwanaadamu.” Ushahidi wa jambo hili ni ushauri ambao Mtume (s.a.w.w) alizoea kuutoa kuhusiana na kutafuta tiba ya baadhi ya maradhi. Ushauri ambao hakuletewa wahyi ila ni kutokana na uzoefu alioupata kutokana na kuishi katika mazingira ya kibinaadamu. Ametaja Abu Daud katika Isnadi yake, kutoka kwa Usama kwamba: “Nilikwenda kwa Mtume (s.a.w.w) naye alikuwa ameketi na maswahaba zake, nao walikuwa (wametulia) Siku moja Mtume (s.a.w.w) alimtembelea mgonjwa, akawaambia nduguze, “Mwiteni daktari,” mmoja wao akasema, “hata nawe pia wasema hivyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?!” Mtume akasema: “Ndiyo, kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuumba maradhi ila ameumba na dawa yake.” Kitendo cha Mtume (s.a.w.w) cha kuwataka ndugu za wagonjwa kumwita daktari kinaonyesha kwamba utabibu wa madawa si miongoni mwa mambo aliyofunuliwa (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na ni kwa sababu hii ndipo akawashauri watu kufuata ushauri wa daktari pale unapohitajika. Pia hali hiyo inahusiana na jinsi alivyokuwa akivaa na kula, ilivyokuwa ikilingana na tabia za wakati wake na mahali alipoishi. Na lau Kwa hivyo basi, Sunnah (Hadith) inafafanua Qur’ani, inachambua hukumu zake, inaikamilisha, inaelezea na kuamua kuhusu mipaka ambayo inatawala kanuni zake kamili, na inafafanua sehemu zenye kutatanisha. Na endapo itaongezea chochote, ziada hiyo haiwezi kupingana na misingi ya kanuni za Qur’ani. Kwa hivyo uhusiano wa Sunnah na Qur’ani ulivyo ni
|