TAREHE YA KIISLAMU 02Deprecated: Function eregi_replace() is deprecated in /home/swaalshia/public_html/page.php on line 99 Deprecated: Function split() is deprecated in /home/swaalshia/public_html/page.php on line 103 BISMMILAHI RAHMANI RAHIYMI Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu Ndoa ya Fatima Zahra na Ali ibn Abi Talib Allah (s.w) aliwapa ushindi Waislamu katika vita vya badr katika mwaka wa 2 wa Hijiria. Miezi miwili baada ya vita hivyo, Fatima Zahra, binti yake Muhammad Mustafa, na Ali, mwana wa Abi Talib walifunga ndoa. Fatima Zahra alikuwa na miaka mitano tu wakati mama yake - Khadija (R.a.), alipofariki, na kuanzia hapo na kuendelea, baba yake, Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.w.) alichukua wajibu wa kazi za mama pia kwa ajili yake. Kifo cha mama yake kilileta pengo katika maisha yake lakini baba yake alilijaza kwa upendo na huruma. Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliweka uangalifu wa hali ya juu kwenye elimu na malezi ya binti yake. Kwa kufanya utii na ibada kwa Allah (s.w.t.) Fatima Zahra alipanda kufikia cheo kikubwa mbele ya Allah (s.w.t.) Wakati Fatima alipokuwa, maswahaba wawili wazee - wa kwanza na kisha baadae mwingine - walimuomba baba yake wamchumbie. Lakini aligeukia pembeni kwa kuchukia, na akasema: "Hili suala la ndoa ya Fatima, binti yangu, liko mikononi mwa Allah (s.w.t.) Mwenyewe, na Yeye pekee ndiye atamchagulia yeye mchumba". Allah (s.w.t.) alifanya uchaguzi Wake
|